Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi
Kigwangalla akiwa na Mkaguzi wa TFDA, Dk. Itikija Mwanga wakiwa nje ya
geti la kituo cha Tabibu Juma Mwaka, Ilala Bungoni, Jijini Dar es
Salaam.
Jengo la Klinini ya tabibu Juma Mwaka linavyoonekana kwa nje
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi
Kigwangalla akiingia kwenye kliniki ya tabibu Juma Mwaka
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi
Kigwangalla akizungumza na mmoja wa watumishi wa kliniki ya Tabibu Juma
Mwaka
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi
Kigwangalla na Mkaguzi wa TFDA, Dk. Itikija Mwanga na Kamanda wa
Polisi, E.M. Swebe wakati wa kufaanya ukaguzi ndani ya kliniki ya Tabibu
Juma Mwaka
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi
Kigwangalla na Mkaguzi wa TFDA, Dk. Itikija Mwanga
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi
Kigwangalla akikagua moja ya orodha ya watu wanaopatiwa kliniki kwenye
kituo hicho
Maafisa wa Polisi na TFDA wakikagua madawa yaliyokutwa ndani ya kituo hicho
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi
Kigwangalla wakiangalia makadi ya wagonjwa ya kliniki yaliyokutwa
nchini humo
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi
Kigwangalla akichungulia moja ya milango iliyofungwa huku wafanyakazi
wakikataa kuifungua
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi
Kigwangalla akiwasikiliza baadhi ya wagonjwa waliofika kupatiwa dawa
wakiwa ndani ya kituo hicho
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi
Kigwangalla akikagua moja ya maeneo ya kliniki hiyo
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi
Kigwangalla wakichungulia ndani kwenye dawa zilizokutwa zinaendelea
kutumika
Baadhi ya madawa yakiwa ndani ya chumba maalum ndani ya kliniki hiyo ya tabibu ya Juma Mwaka
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi
Kigwangalla akiendelea kukagua ndani ya kliniki ya Tabibu Juma Mwaka.
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi
Kigwangalla akichungulia moja ya jengo ndani ya kliniki hiyo ya Tabibu
Juma Mwaka
Moja ya madawa yaliyokutwa ndani ya Kliniki ya Tabibu Juma Mwaka
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi
Kigwangalla akitoa matamko juu ya kuhakikisha Tabibu Juma Mwaka
anajisalimisha mikononi mwa jeshi hilo la Polisi pamoja ndani ya masaa
24.
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi
Kigwangalla akitoa maagizo kwa Jeshi la Polisi kuhakikisha wanaimalisha
ulinzi ndani ya kituo hicho pamoja na kumkamata Tabibu Juma Mwaka kwa
kukiuka taratibu halali za Serikali.
Mkaguzi wa Chakula kutoka Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Dk Itikija Mwanga akizungumza na vyombo vya Habari juu ya tukio hilo pamoja na madawa waliyoyakuta ndani ya kliniki hiyo
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi
Kigwangalla akitoa maagizo juu ya kujisalimisha kwa Tabibu Juma Mwaka
ndani ya masaa 24 kabla ya kuchukuliwa hatua kali kutokana na kukiuka
taratibu za Nchi ikiwemo kuendesha huduma za kitabibu licha ya
kufungiwa. (Picha zote na Andrew Chale, Modewjiblog).
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi
Kigwangalla amefanya ziara ya kushtukiza kwa mara nyingine tena
kwenye kliniki ya Bwana. Juma Mwaka (Dk. Mwaka) ili kufanya ukaguzi wa
kinachoendelea katika kliniki hiyo ambayo hivi sasa imebadilishwa jina
na kuwa kampuni. (Kaama inavyoonekana pichani).
Dk
Kigwangalla ambaye amefanya ziara ya kushtukiza katika kliniki hiyo
kama alivyowahi kufanya mara baada ya kuteuliwa kushika wadhifa huo
ambapo katika tukio la awali, ilielezwa kuwa Dk. Mwaka alikimbia na
kumuachia Ofisi Naibu Waziri na baadae aliweza kuibuka tena na kuendelea
naa shuguli zake hizo.
Hivi
karibuni Julai 11 mwaka huu, mamlaka husika ziliweza kutangaza
kumfungia Dk. Mwaka juu ya kuendelea na shughuli zake hizo ikiwemo
kumfutia kibali chake ambapo baada ya siku mbili alirudia tena kufanya
shughuli zake huku akibadilisha jina kutoka Kliniki na kuwa kampuni.
Tukiolilianza
saa sita kasoro robo, ya mchana ambapo Dk Kigwangalla alifika eneo la
Dk. Mwaka huku akikuta geti likiandwa limefungwa (Closed), licha ya
ndani kuwa na watu wakiendelea na shughuli za tiba.
Ndani,
ya kituo hicho kulikutwa na wafanyakazi watatu akiwemo Mwanaume mmoja
na wanawake wawili ambao baada ya kuulizwa wahusika wakuu, wafaanyakazi
hao walikana kuwapo mahala hapo ndipo Polisi walipotumia mamlaka ya
kisheria ya kuamuru kufanya ukaguzi pamoja na Mamlakahusika wakiwemo
TFDA, Baraza la Famasia Nchini na lile la Baraza la Tiba Asili na Tiba
mbadala pamoja na Dk. Kigwangalla.
Baada
ya uchunguzi wa kina ndani ya kituo hicho, walikuta madawa mbalimbali
yakiwemo ya yanayotumika mahospitali huku mengine yakiwa yamesha kwisha
muda wake. Mbali na dawa hizo, pia walikuta nyaraka mbalimbali za watu
waliokuwa wanafika kwenye kituo hicho kupata tiba licha ya kufungiwa.
Aidha,
Dk. Kigwangalla na timu yake hiyo walifanikiwa kukuta shehena kubwa ya
madawa ya mitishamba ambayo imehifadhiwa kwenye chumba maalum hata
hivyo, Dk. Kigwangalla alitaka dawa hizo ishikiliwe.
"Dk.
Mwaka', naagiza akamatwe mara moja, ndani ya masaa 24, na afikishwe
mahakamani kwa kukaidi agizo halali la Serikali la kusitisha huduma zake
za tiba asili na tiba mbadala, impersonation kwa kujifanya yeye ni
Daktari Bingwa wa Tiba ya kisasa wa Magonjwa ya Wanawake.
Hii
ni pamoja na kukutwa na shehena ya dawa za tiba ya kisasa za aina ya
'ferrovit ' bila kuwa na vibali vya serikali, na pia kukutwa na shehena
ya dawa za tiba asili na tiba mbadala bila kuwa na kibali, baada ya
kibali chake cha utabibu kufutwa na Serikali Julai 11, 2016” alieleza
Dk. Kigwangalla.
Dk.
Kigwangalla ametoa maagizo ya moja kwa moja kwa Mrakibu wa Polisi
kutoka Kituo cha Polisi Ilala, ambaye alikuwa kwenye zoezi hilo,
Kamanda, E. M Swebe ambaye hata hivyo aliahidi kushughulikia suala
hilo.
Kwa upande wake mkaguzi
wa TFDA, Dk. Itikija Mwanga amesema kuwa, madawa yaliyokutwa
yataendelea kushikiliwa hii ni pamoja na kufanyiwa utafiti kama ni kweli
yanafaa kwa matumizi ya kibinadamu ama la pamoja na taratibu zingine.
No comments:
Post a Comment