Mmoja
wa wanafunzi hao ambaye jina lake limehifadhiwa akiwa akiwa anasomewa
ujumbe na mwalimu mmoja wapo namna walivyokuwa wakichati na mwalimu
jumbe za mapenzi
Mmoja wa walimu akiwa anamsomea mzazi mambo ambayo mwanae alikuwa akiwasiliana na moja ya walimu wa shule hiyo
Hizi ni Baadhi ya karatasi ambazo waliandika walimu wanaotembea na wanafunzi na kubainika mwalimu mmoja anatembea na zaidi ya mwanafunzi mmoja
Diwani wa kata hiyo ambayo haikufahamika mara moja Bw. Pantaleo Lyakurwa aliyekaa akiwa anasikiliza mashitaka hayo
Mmoja wa walimu akiwa anamsomea mzazi mambo ambayo mwanae alikuwa akiwasiliana na moja ya walimu wa shule hiyo
Hizi ni Baadhi ya karatasi ambazo waliandika walimu wanaotembea na wanafunzi na kubainika mwalimu mmoja anatembea na zaidi ya mwanafunzi mmoja
Diwani wa kata hiyo ambayo haikufahamika mara moja Bw. Pantaleo Lyakurwa aliyekaa akiwa anasikiliza mashitaka hayo
Na mwandishi wetu Blogs za Mikoa
Walimu
wanne ambao majina yao yamehifadhiwa kwa sasa wamekamatwa wakiwa na
mahusiano ya kimapenzi na Mabinti wa shule mojawapo ya Sekondari iliyopo
wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro ambayo pia jina lake limehifadhiwa.
Walimu
hao wamebainika baada ya kufanyika msako mkali wa kukamata wanafunzi
wanaotumia simu za kiganjani kinyume na utaratibu wa shule hiyo, ambapo
walikagua ujumbe mfupi wa maneno yaani SMS kwenye simu hizo ndipo
walipokuta walimu hao wakiwasiliana na wanafunzi hao kwa meseji
zilizoashiria mapenzi.
Baada
ya kupata taarifa hizo Diwani wa eneo hilo Bw. Pantaleo Lyakurwa
alifika na Askari wa Jeshi la Polisi katika shule hiyo na kuwakamata
walimu wawili ambapo wamefikishwa Polisi na walimu wengine wawili bado
wanasakwa.
Bwana
Lyakurwa amewaonya vikali walimu ambao wanaendelea na tabia za kutembea
na wanafunzi na kutoa agizo kuwa atakayebainika atakamatwa na
kufikishwa Polisi, Mahakamani kisha kusimamishwa kazi.
Wakati
huo huo kuna Binti wa miaka 15 kidato cha kwanza ambaye pia alikamatwa
akitembea na mmoja wa walimu hao aliwaacha watu mdomo wazi baada ya
kugundulika kuwa ni mjamzito lakini cha ajabu aligoma kumtaja mtu
aliyempa ujauzito huo.
No comments:
Post a Comment