Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo au Habari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @fredynjejephotography Twitter @Fredynjeje
Tanzania imepiga hatua kubwa katika kuboresha
huduma za uzazi wa mpango nchini tofauti na kipindi cha nyuma ili kuweza
kuondoa idadi ya ongezeko kubwa la watu na kupunguza vifo kwa wajawazito na
watoto kama sera ya Afya ya mwaka 2007 inavyosema.
Hayo yamesemwa na Waziri Ummy Mwalimu(Mb) hivi
karibuni wakati akifungua mkutano wa Bodi kwa nchi zilizoamua kuongeza idadi ya
watu wanaofahamu uzazi wa mpango kundi linalojulikana kama "FP 2020
Reference Group.
“Tanzania imepiga hatua kubwa katika kuboresha
huduma za uzazi wa mpango nchini tofauti na kipindi cha nyuma ili kuweza
kuondoa idadi ya ongezeko kubwa la watu na kupunguza vifo kwa wajawazito na
watoto kama sera ya Afya yam waka 2007 inavyosema” alisema Waziri Ummy.
Aidha Waziri Ummy amesema kuwa mkutano huu
unafanyika kwa mara ya kwanza barani Afrika na hususani katika ardhi ya
Tanzania hii ni kutokana na mafanikio makubwa yaliyofikiwa katika eneo hili la
uzazi wa mpango .
Waziri Ummy amesema kuwa mafanikio hayo ni pamoja
na ongezeko la bajeti katika eneo la uzazi wa mpango na kupunguza hali
utegemezi kwa kiasi kikubwa kutoka kwa wahusani,kuimarisha mìfumo ya usambazaji
wa dawa na vifaa tiba za uzazi wa mpango hapa nchini
Mbali na hayo Waziri Ummy alieleza kuwa katika
mikoa ya kanda ya ziwa na magharibi mwa
nchi kumekuwa na ongezeko la uelewa na utumiaji wa huduma za uzazi wa mpango
kama vile mkoa wa Mara kuna ongezeko la utumiaji kutoka asilimia 10 hadi
asilimia 29 kuanzia mwaka 2010 hadi 2015 na katika mkoa wa kagera kumekuwa na
ongezeko kutoka asilimia 24 hadi asilimia 39.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la
Umoja wa Mataifa linalosimamia masuala ya uzazi wa mpango Dkt.Babatunde alipongeza juhudi zinazofanywa na Serikali
ya nchi yetu katika kuhakikisha huduma
hii inaimarika.
Mkutano huo wa siku tano ulioanza Oktoba 31
hadi Novemba 4 mwaka huu unahudhuriwa na
wajumbe na wadau kutoka nchi mbalimbali duniani ikiwa na lengo la kujadili fursa
mbalimbali na changamoto zilizopo katika eneo la afya ya uzazi wa mpango
duniani.
No comments:
Post a Comment