Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo au Habari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @fredynjejephotography Twitter @Fredynjeje
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein akiongea na wananchi wakati
wa sherehe za miaka 53 ya mapinduzi ya Zanzibar ambapo alisema mbali za
jitihada zilizofanywa na serikali hiyo katika kuinua maisha ya
wazanzibar ameahidi kuendelea kusimamia rasilimali ili zitumike kwa
maslahi ya wananchi wote.
2-Makamo wa Pili wa Rais Zaznzibar
Balozi Seif Ali Idd akiongea na wananchi wakati wa sherehe za miaka 53
ya mapinduzi ya Zanzibar ambapo alisema serikali ya mapinduzi ya
Zanzibar itaendelea kuweka jitihada ili kuendelea kujenga uchumi za
Zanzibar kwa maslahi ya wananchi.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein akiwasalimia wananchi
walijitokeza katika sherehe za miaka 53 ya mapinduzi ya Zanzibar
zilizofanyika katika uwanja wa Amani, Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein akiimba wimbo wa Taifa katika
sherehe za miaka 53 ya mapinduzi ya Zanzibar zilizofanyika katika
uwanja wa Amani, Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein akikagua gwaride katika
sherehe za miaka 53 ya mapinduzi ya Zanzibar zilizofanyika katika uwanja
wa Amani, Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein akisalimiana na viongozi
wastaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar katika sherehe za miaka 53 ya mapinduzi ya
Zanzibar zilizofanyika katika uwanja wa Amani, Zanzibar.
Vikundi mbalimbali, Asasi za
Kiraia,Vyama vya Siasa,Mikoa,Wizara na Taasisi za Serikali wakipita
mbele Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali
Mohamed Shein katika sherehe za miaka 53 ya mapinduzi ya Zanzibar
zilizofanyika katika uwanja wa Amani, Zanzibar.
Vikosi mablimbali vya Jeshi la
Polisi vikipita mbele Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein katika sherehe za miaka 53 ya mapinduzi
ya Zanzibar zilizofanyika katika uwanja wa Amani, Zanzibar.
Vijana vya halaiki wakiwa katika
umbo linaloonesha miaka 53 ya mapinduzi ya Zanzibar katika sherehe
zilizofanyika katika uwanja wa Amani, Zanzibar.
Kikosi cha Kwata la KimyaKimya
wakionesha onesho wakati wa sherehe za miaka 53 ya mapinduzi ya Zanzibar
zilizofanyika katika uwanja wa Amani, Zanzibar.
Komando wa Jeshi la Wananchi
Tanzania akishuka katika kamba katika sherehe za miaka 53 ya mapinduzi
ya Zanzibar zilizofanyika katika uwanja wa Amani, Zanzibar.
Kikosi cha Makomandoo wa Jeshi la
Wananchi Tanzania wakionesha onesho wa namna ya kuakibiana na vikwazo
mbalimbali wawapo kazini katika sherehe za miaka 53 ya mapinduzi ya
Zanzibar zilizofanyika katika uwanja wa Amani, Zanzibar.
Askari wa Kikosi cha Mbwa,
akionesha namna mbwa anavyoweza kuruka vikwazo mbalimbali katika
kukabiliana na wahalifu katika sherehe za miaka 53 ya mapinduzi ya
Zanzibar zilizofanyika katika uwanja wa Amani, Zanzibar.
………..
Na: Frank Shija – MAELEZO
ZANZIBAR imeadhimisha miaka 53
ya Mapinduzi Matukufu huku ikiwa imepiga hatua mbalimbali za
kimaendeleo na utoaji wa huduma bora za kijamii.
Hayo yamebainishwa na Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein
wakati akihutubia wananchi katika sherehe za maadhimisho ya Mapinduzi
leo katika uwanja wa Amani, Unguja, Zanzibar.
Dkt. Sein amesema kuwa siku ya
Mapinduzi ni muhimu sana katika historia ya Zanzibar kwani ndiyo siku
ambayo Wazanzibar walipokuwa huru katika nchi yao na kuweza kufanya
shughuli mbalimbali za kujiletea maaendeleo.
“Tukiwa tunasherehekea miaka 53 ya
Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ni vyema tukajivunia maendeleo
yaliyopatikana na yanayoendelea kupatikana.”Alisema Dkt. Shein.
Akitaja baadhi ya mafanikio
yaliyopatikana tangu Mapinduzi Matukufu yatokee tarehe 12 Januari 1961,
Dkt. Shein amesema kuwa mafanikio makubwa yamepatikana katika sekta za
elimu kwa kuwa na ongezeko la shule kutoka shule 752 mwaka 2015 hadi
kufikia 843 mwaka 2016.
Ongezeko hilo limeenda sambamba na
ongezeko la udahili wa wananfunzi ambapo umeongezeka kutoka wanafunzi
384,000 hadi kufikia 424,000 mwaka 2016.
Katika sekta ya afya kumekuwa na
mafanikio ya kuongezeka kwa vituo vya afya kwa asilimia 13.4 ambapo
mwaka 2015 kulikuwa na Vituo vya Afya 134 hadi kufikia sasa jumla ya
Vituo 152 vimepatikana.
Mafanikio mengine ni pamoja na
upatikanaji wa ajira 2658 zilizotokana na miradi mbalimbali
iliyozindulia katika kipindi hiki cha maadhimisho ya siku ya Mapinduzi,
kukua kwa Sekta ya Utalii kwa ongezeko la watalii kwa asilimia 13 huku
ikichangia pato la taifa kwa asilimia 27.
Huduma za kijamii zimezidi
kuboreshwa huku upatikanaji wa maji safi na salama umeendelea kutatuliwa
ambapo miradi ya maji imeekuwa ikitekelezwa ikiwemo kuchimba visima
vipya 9 na kuvifanyia ukarabati visima vya zamani.
Kwa upande wake Makamu wa Pili wa
Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd amesema kuwa
Mapinduzi haya yamekuwa chachu ya kuleta maendeleo kwa kuwa yamewaweka
Wazanzibar kuwa huru katika kutekeleza shughuli zao za kujiletea
maendeleo.
Zanzibar imeadhimisha miaka 53 ya
Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar huku ikiwa imepiga hatua kubwa za
kimaendeleo ambapo katika shamra shamra za maadhimisho haya jumla ya
miradi 32 ya maendeleo imezinduliwa huku mingine 16 ikiwekwa jiwe la
msingi tayari kwa utekelezaji wake, hayo yote ni matunda yatokanayo na
Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ambayo baadaye yalizaa Muungano wa
Tanganyika na Zanzibar.
No comments:
Post a Comment