Mkuu
wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda, akionyesha majina mengine 97
ya wafanyabiashara wa Dawa za Kulevya awamu ya tatu wakati akimkabidhi
majina hayo Kamishna Mkuu
wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Rogers William
Sianga, kwa ajili ya kuyafanyia kazi. Makonda alikabidhi majina hayo leo
mchana wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika kwenye
Ukumbi wa Mwalimu Nyerere (JNCC) jijini Dar es Salaam, ambapo alisema kuwa majina ya awamu hii ya tatu yatatikisa
nchi kwani wameanzia toka uongozi wa awamu ya tatu iliyoongozwa na Rais
Mstaafu,Benjamini Mkapa, ya nne Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete na
hii ya Tano inayoongozwa na Rais Dk. John Pombe Magufuli.
CHANZO MAFOTO BLOG
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda akikabidhi majina
mengine 97 ya awamu ya tatu kwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na
Kupambana na Dawa za Kulevya,
Rogers William Sianga
ili yaanze kushughulikiwa.
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda akizungumza katika
mkutano huo amekabidhi majina mengine 97 ya awamu ya tatu kwa Bw. Rogers
William sianga kuwa kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na
Dawa za Kulevya ili yaanze kushughulikiwa.
Shekh wa Mkoa wa Dar es salaam na Mwenyekiti wa Kamati ya Amani Alhadi
Mussa akizungumza na watendaji mbalimbali wa vyombo vya ulinzi na
usalama mkoa wa Dar es salaam pamoja na viongozi mbalimbali wa Chama cha
Mapinduzi, Wenyeviti wa serikali za mitaa na madiwani pamoja na vijana
mbalimbali waliokuwa wanatumia dawa za kulevya katika mkutano wa taarifa
ya maendeleo ya Kampeni ya kupiga vita dhidi ya madawa ya kulevya.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Khalid Mohamed, TID, akizungumza na
kutoa ushuhuda, na kuahidi kutoa ushirikiano katika Vita ya kupambana na
madawa ya kulevya.
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh. Paul Makonda akizungumza
jambo na Bw. Rogers William sianga kuwa kamishna Mkuu wa Mamlaka ya
Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya katika mkutano wa kutoa tathmini
ya kampeni ya kutokomeza madawa ya kulevya Kamishna katika mkoa wa Dar
es salaam.
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda akiwa pamoja na viongozi wengine wakiwa katika mkutano huo.
Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es salaam Kamishna Saimon Sirro akizungumzo wakati akitoa taarifa ya kampeni hiyo leo.
No comments:
Post a Comment