Social Icons

Monday 10 April 2017

VIJANA WATAKIWA KUWA MSTARI WA MBELE KATILETA MAENDELEO YA BARA LA AFRIKA

Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo au Habari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @fredynjejephotography Twitter @Fredynjeje
 Naibu Waziri wa Afya Wanawake Jinsia na Watoto , Dk Hamisi Kigangwala akifungua Kongamano la Vijana barani afrika juu ya Maendeleo barani Afrika.

 Washiriki wa Kongamano hilo Vijana kutoka nchi Mbalimbali  wakifatilia Hotuba ya Dk Kigwangala


Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii
Vijana barani Afrika wametakiwa kuwa mstari wa mbele katika  kueleta Maendeleo hili kufikia malengo hasa katika kipindi hiki cha mapinduzi ya Teknolijia na Viwanda.

Hayo yamesemwa leo na Naibu Waziri wa Afya Wanawake Jinsia na Watoto, Dk .Hamisi Kigwangalla alipokuwa akifungua kongamano la Vijana barani Afrika lililoandaliwa na Tasisi ya Uongozi Institute jijini Dar es Salaam.

Akizungumza kwa Niaba ya Makamu wa Rais Kigwangala amesema kuwa mara zote vijana wanapokusanyika na kujadili maendeleo ya bara la Afrika ni muhimu sana kwani leo vijana ndio wadau wakubwa katika swala zima la maendeleo ya bara lao  .

“inaeleweka kabisa ukuaji wa bara la Afrika unategemea vijana ndio maana ajenda ya 2063 inahusisha ubunifu , Nishati , utamaduni na swala zima la siasa safi  kama serikali tunawahimiza vijana kujitambua na kuwawezesha  kufikia malengo hili kuweza kupambana na vikwazo vinavyo wakabili” amesema Kigwangala.

Ameongeza kuwa vijana wanatakiwa kutambua vikwazo vinavyo wakabili kama fursa ya kujipatia maendeleo kwa kutatua vikwazo hivyo kwa ajili ya maendeleo ya vijana wa kesho.

Amesema mjadala wa leo sio tu kwa ajili ya Vijana bali ni kwa ajili ya maendeleo ya bara la Afrika kwa kuwa na sera zitakazowawezesha vijana.


 Rasi wa Vijana Barani Afrika , Francine Muyumba  akizungumza na Vijana mbalimbali kutoka nchi mbalimbali ambao walishiriki kongamno hilo la Vijana

 washiriki wa Kongamano wakisikilza kwa makini
 Mmoja wa Vijana kutoka nchini Nigeria, Arinze Obiezue  akitoa neno la shukrani kwa naiba ya washiriki wa kongamano hilo.
 Viongozi wa meza kuu wakiongoza na Naibu Waziri wa Afya , Dk Hasmisi Kigwangalla  wakisikila maneno ya shukrani kutoka kwa kijana
Picha ya pamoja ya Naibu Waziri na Washiriki wa Kongamano hilo

No comments: