Social Icons

Wednesday 23 August 2017

OXFAM NA TALA WAWAKUTANISHA WADAU KUJADILI NAMNA WATAKAVYOFANYA KAMPENI YA HAKI YA ARDHI KWA WANAWAKE

Bi. Eluka Kibona Mkuu wa kitengo cha Ushawishi na utetezi kutoka Shirika la Kimataifa la Oxfam Tanzania, Akifungua mkutano na kuelezea madhumini yake kwa niaba ya Mkurugenzi Mkazi wa Oxfam Bw.Francis Odokorachi.

Mratibu wa NES  Bw. Benard akielezea namna wanavyofanya kazi na wadau wengine katika maswala ya ardhi, ambapo alielezea kwa undani namna ya kuangalia haki za wanawake katika umiliki wa Ardhi,pamoja na hayo aliongeza kuwa wanafanya kazi pamoja na mashirika 14 wakiwemo Oxfam na TARA. Mwisho alieleza kipaumbele chao ni kampeni katika mambo yanayohusiana na Ardhi.
Profesa Majourin Mbilinyi Mwanamke Mwanaharakati,akielezea kuhusu jinsia na ukombozi kwa wanawake, alisema mwanake hawezi kukomboka bila kuwa mkombozi wa jamii, alisema kuwa ni muhimu sana kuwakomboa wanawake wadogo wadogo ambao wanazalisha chakula ili wawe na haki ya umiliki wa Ardhi .
 Baadhi ya wajumbe wakiendelea kufuatilia na kuchukua mambo mbalimbali muhimu katika mkutano huo uliowakutanisha wadau mbalimbali kujadili namna watakavyofanya kampeni ya haki ya wanawake katika kumiliki Ardhi.
 Bi. Eluka Kibona Mkuu wa kitengo cha Ushawishi na utetezi kutoka Shirika la Kimataifa la Oxfam Tanzania, akizungumzia umuhimu wa wanawake katika kumiliki ardhi kwa sababu mwanamke anashiriki kwa asilimia kubwa katika kuzalisha Chakula na kutengeneza bidhaa mbalimbali katika kujipatia kipato, alisema kuwa ni muhimu kwa wanawake kuwa na haki sawa katika umiliki wa ardhi na pia mashirika ya kimataifa kushirikiana na wazawa katika kuhakikisha mambo yanayohusiana na ardhi yanaenda vizuri.
Mratibu wa Miradi ya Ardhi kutoka Care International Bi. Mary Ndaro akielezea kuhusu idadi kubwa wanawake wanaozalisha mazao ya chakula wanaishi vijijini na wanategemea Ardhi katika swala zima la maendeleo na kujipatia kipato katika kuendesha maisha yao, aliongeza kuwa ili kampeni hii iendelee wanawake wanahitaji  msaada wa karibu.
Mratibu wa Miradi ya Ardhi kutoka Shirika la Kimataifa la Oxfam Tanzania Bi. Naomi Shadrack akizungumza namna akielezea namna wanavyofanya kazi kuhusiana na maswala ya ardhi na ushiriki wao katika kampeni ya wanawake katika kumiliki ardhi
Bi. Josephine Dungumaro(Kulia) Mshauri wa Jinsia kutoka Shirika la kimataifa la utafiti wa Mifugo akielezea namna shirika lao linavyofanya kazi na kugusia maeneo wanayofanyia kazi ni pamoja na Kiteto,Chalinze na Bagamoyo.
Bi. Amina Ndiko(Kulia) kutoka Oxfam akisisitiza jambo kuhusu maswala ya wanawake na umiliki wa Ardhi.
Mwezeshaji Bw. Evans Rubara akiendelea kutoa Mwongozo 
 Bi Nuria Mshare akiwasilisha Mada iliyohusu 'Harmonization of Land Laws'
 Mshiriki wa Shindano la Mama Shujaa Msimu wa nne Bi. Edna Kiogwe akiwasilisha mada juu ya 'Elimu ya wanawake kujua haki zao za ardhi'
Bi. Wigayi Kisandu Mwanasheria kutoka WLAC, amezungumza namna ya wanawake wanavyopewa nafasi ndogo katika kumiliki ardhi na kufanya juhudi za kuhakikisha wanapata nafasi ya kumiliki ardhi.
 Mkutano ukiendelea
Picha zote na Fredy Njeje/ Blogs za Mikoa Tanzania.

No comments: