Hugoline Martin Mtambachuo jina maarufu
kama DJ CHOKA anatarajia kuachia wimbo wake mpya alioupa jina la BILA
SABABU ukiwa umefanyika pale Mbagala kwa Prod Dupy. DJ Choka amesema
ameamua kuachia wimbo huo tarehe hiyo kwa sababu ni tarehe ya kumbukumbu
yake ya kuzaliwa.
Wimbo huu utakuwa wimbo wa kwanza kuutoa
kwa mwaka huu 2017 toka ameinuka kutoka kitandani kwa kujiuguza ugonywa
wa KIFUA KIKUU (TB) kwa takribani miezi 6 hadi 8. Wimbo wa mwisho
kuuachia ulikuwa unaitwa NITALALA UZEENI ambapo aliuachia mwaka 2014
uliokuwa umewashirikisha wasanii kama COUNTRY BOY, YOUNG LUNYA, B GWAY
na CLIMAX BIBO chini ya Prod Gard kutoka A.M Rec.
Wasanii walioshirikishwa kwenye wimbo huu
mpya amesema ni mapema kuwataja kwa sasa lakini wimbo ukitoka
watajulikana, anaomba mashabiki kuupokea ujio huu mwingine mpya kutoka
kwake pamoja na nyingine zitakazo kuja.
No comments:
Post a Comment