Social Icons

Sunday 10 September 2017

UJIO MWINGINE MPYA KUTOKA KWA DJ CHOKA NDIO HUU

Inline image

Hugoline Martin Mtambachuo jina maarufu kama DJ CHOKA anatarajia kuachia wimbo wake mpya alioupa jina la BILA SABABU ukiwa umefanyika pale Mbagala kwa Prod Dupy. DJ Choka amesema ameamua kuachia wimbo huo tarehe hiyo kwa sababu ni tarehe ya kumbukumbu yake ya kuzaliwa.
Wimbo huu utakuwa wimbo wa kwanza kuutoa kwa mwaka huu 2017 toka ameinuka kutoka kitandani kwa kujiuguza ugonywa wa KIFUA KIKUU (TB) kwa takribani miezi 6 hadi 8. Wimbo wa mwisho kuuachia ulikuwa unaitwa NITALALA UZEENI ambapo aliuachia mwaka 2014 uliokuwa umewashirikisha wasanii kama COUNTRY BOY, YOUNG LUNYA, B GWAY na CLIMAX BIBO chini ya Prod Gard kutoka A.M Rec.
Wasanii walioshirikishwa kwenye wimbo huu mpya amesema ni mapema kuwataja kwa sasa lakini wimbo ukitoka watajulikana, anaomba mashabiki kuupokea ujio huu mwingine mpya kutoka kwake pamoja na nyingine zitakazo kuja.

No comments: