Mkuu
wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi akisalimiana na Mwenyekiti wa
klabu ya wafanyabiashara wateja wa NMB Singida Emmanuel Rweyemamu Kyoma
mapema leo kabla ya kufungua warsha ya siku moja ya klabu hiyo, katika
ukumbi wa Kanisa Katoliki mjini Singida.
Mkuu
wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi akikagua baadhi ya bidhaa za
wafanyabiashara wateja wa NMB Singida mapema leo kabla ya kufungua
warsha ya siku moja, katika ukumbi wa Kanisa Katoliki mjini Singida.
Meneja
wa NMB Kanda ya kati Straton Chilongola akizungumza klabu ya
wafanyabiashara wateja wa NMB Singida mapema leo wakati wa ufunguzi wa
warsha ya siku moja, katika ukumbi wa Kanisa Katoliki mjini Singida.
Wafanyabiashara
wateja wa NMB Singida wakiwa katika warsha ya siku moja katika ukumbi
wa Kanisa Katoliki mjini Singida mapema leo.
………………………………………………………………………
Benki
ya NMB imetakiwa kuwasaidia wafanyabiashara Mkoani Singida kuanzisha
kiwanda cha kutengenea vifungashio, ili waweze kuhifadhi bidhaa zao
katika ubora unaokubalika kitaifa na kimataifa.
Mkuu
wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi ametoa rai hiyo mapema leo wakati
akifungua warsha ya siku moja ya klabu ya wafanyabiashara wateja wa
NMB, katika ukumbi wa Kanisa Katoliki mjini Singida.
Dkt
Nchimbi amesema klabu hiyo ya wafanyabiashara itaweka alama kubwa
katika maendeleo endapo watajipanga na kuanzisha kiwanda cha kutengeneza
vifungashio hivyo kuliko kuendelea kuvifuata nje ya Singida au nje ya
nchi.
“Uzoefu
usipotumika vizuri unaweza ukawa kikwazo cha kuendelea, msizoee kufuata
vifungashio na label nje ya singida wakati fursa ipo ya kuanzisha
kiwanda hicho Singida”, amesema na kuongeza kuwa,
“Wafayabiashara
mzipende biashara zenu na kuziweka katika hali ya usafi na yenye
kuvutia, wengine wanapenda kujisafisha na kujipendezesha wenyewe lakini
ukiangalia biashara zao hazivutii, zimewekwa tu bila kufungashwa
vizuri”, amesisitiza.
Aidha
amewataka wafanyabiashara wasiogope kukopa kwakuwa sio jambo la aibu
wala fedheha, ila kinachotakiwa ni kuwa na nidhamu ya mkopo na malengo
ili waweze kufanikiwa.
“Akina
mama jifunzeni kuwa na nidhamu ya mkopo, sio unakopa leo mara unasikia
kapu la mama, jifikirie hayo ndio malengo ya huo mkopo hata kama ni
jambo muhimu?, nidhamu ya mkopo inatakiwa ianze kabla ya kukopa na
iendelee kuwepo.
Dkt
Nchimbi pia ameishukuru benki hiyo kwa kushirikiana na serikali katika
mambo mbalimbali ya kielimu na afya, pia amewashukuru kwa kutoa mikopo
kwa watumishi wa umma jambo ambalo linawasiadia katika mambo mbalimbali.
Naye
Meneja wa NMB Kanda ya kati Straton Chilongola amesema klabu za
wafanyabiashara nchini ziko 34 ambazo zimekuwa zikipatiwa mafunzo mikopo
kutoka katika benki hiyo.
Chilongoloa
amesema benki hiyo imekuwa ikitoa mafunzo juu ya ulipaji kodi,
ujasiriamali, masuala ya mitaji, leseni na ardhi ili wafanyabiashara hao
waweze kukuza mitaji yao.
Amesema
benki hiyo imefanikiwa kuwakuza wafanyabiashara wengi ambazo wameanza
nao wakiwa wafanyabiashara wadogo ambapo sasa wamekuwa wakubwa na wakati
huku wakiajiri wengine na hivyo kukuza uchumi.
Kwa
upande wake Mwenyekiti wa klabu ya wafanyabiashara wateja wa NMB
Singida Emmanuel Rweyemamu Kyoma amesema wazo la kuanzisha kiwanda cha
kutengeza vifungashio wamelipokea vizuri huku wakijipanga kuandaa andiko
kwa ajili ya kiwanda hicho.
Kyoma
amesema kwa ushirikiano na NMB kiwanda hichokitaweza kujengwa Singida
huku wakimuahidi Mkuu wa Mkoa kuwa Mkoa wa Singida utazalisha chakula
cha kutosha kulisha Mkoa wa Dodoma.
Amesema
benki ya NMB imekuwa ikishirikiana na wafanyabiashara hao hivyo mipango
ya kukuza uchumi kama huo wa kuanzisha viwanda utatekelezeka bila
matatizo yoyote.
No comments:
Post a Comment