Social Icons

Tuesday 24 October 2017

NMB YATOA MSAADA WA BATI 300 KWA SHULE ILIYOENZULIWA NA MVUA NA KOMPYUTA KWA SHULE ZA SEKONDARI .

FOCUS LUBENDE  MENEJA  MAHUSIANO  BIASHARA  WA  BENKI YA NMB KANDA YA NYANDA ZA JUU AKIMKABIDHI MKUU WA MKOA WA KATAVI  MEJAGENERALI  MSTAAFU  RAPHAEL MUHUGA   KOMPYUTA     7 ZILIZOTOLEWA  MSAADA NA  BANK YA NMB KWA AJILI YA SHULE NNE ZA SEKONDARI ZA    HALMASHAURI YA MPIMBWE WILAYANI MLELE  MSAADA HUO ULIKABIDHIWA  HAPO JANA KWENYE  HAFLA ILIFANYIKA KATIKA OFISI YA  HALMASHAURI YA  MPIMBWE NA KUHUDHURIWA NA VIONGOZI KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WA MKOA WA KATAVI NA WAWILAYA YA MLELE WALIONGOZWA NA MKUU WAO WA WILAYA YA MLELE  RACHEL KASANDA  PAMOJA NA MADIWANI







Na  Walter  Mguluchuma.
          Katavi .
Benki ya  NMB   imetowa  msaada wa   Bati 300 zenye  thamani za  Tshs 8,000,000 kwa ajili ya  shule  ya Msingi  Kilida iliyoko   katika  Halmashauri ya Mpimbwe  Wilaya ya  Mlele  Mkoa wa  Katavi   ambayo   majengo ya  madarasa ya Shule hiyo yalienzuriwa na mvua  na  Kompyuta 7 kwa ajiri ya Shule  tatu za  Sekondari   kwenye  Halmshauri hiyo .
  Msaada  huo  ulikabidhiwa  hapo   kwa  Mkuu wa  Mkoa wa  Katavi  Meja  Generali  Mstafu  Raphael Muhuga  na  Govemment Ralationship Manenger   Meneja  Mahusiano  Biashara  ya  Serikali wa  NMB  wa   Kanda  za  Nyanda  za  Juu  Focus Lubende  kwa niaba ya  uongozi wa    Benki  ya  Nmb   katika  Hafla iliyofanyika  katika   viwanja   vya  Halmashauri ya  Mpimbwe.
 Focus   alisema   uongozi wa   Mkoa wa  Katavi  ulitambua  kabisa  kuwa  NMB  ni  Benki  iliyokaribu  na  Wananchi  na  hivyo  kuwa ni sehemu ya kwanza  ya kukimbilia  ili kutatua  changamoto  ya majanga ya mvua  yalioleta madhara  makubwa  katika Wilaya ya Mlele .
 Wao  kama  NMB   walipata maombi ya   kuombwa msaada  kupitia kwa Mkuu wa Wilaya ya Mlele  walifarijika  na kuamua  mara  moja  kuja kushirikiana  na Mkoa wa Katavi  kunusuru  maisha ya  watu  wakati wa  janga  la mvua zilizoharibu  majengo na miundo mbinu  mbalimbali  katika   Vjiji vya  Kasansa na  Kilida  Wilayani Mlele .
Alishukuru kwa  wao  kutambuliwa  kuwa   NMB  ni  mahali sahihi  ,hii inaonyesha  thamani  kwa  kutambuliwa kwa michango yao wanayoitowa kwenye jamii kama   benki inayochangia  maendeleo.
 Alisema  vifaa  hivyo  walivyovikabidhi  ni  sehemu  ya ushiriki  wao katika  maendeleo ya jamii na wao kama  benki  inayoongoza   Tanzania kw a  kuwa na matawi mengi   wanahakikisha  jamii inayowazunguka  inafaidika  kutokana  na  faida  wanayoipata.
Wanafahamu  kuwa  Shule ya Msingi Kilida  ilipata   janga la  kuenzuliwa  paa   lake  la majengo ya madarasa  hivyo kufanya  mazingira  ya wanafunzi  kuwa magumu .
 Alisema  benki hiyo  inatambua  mabati hayo waliotowa  yatarejesha  tabasamu  kwa wanafunzi ,walimu  na  jamii nzima  ya Kilida  na  Mlele   na  kwa  wanakazi  wote kwa ujumla wake .
Mkuu wa  Wilaya ya  Mlele   Rachel  Kasanda  alisema kuwa     msaada huo wa  bati utasaidia kurekebisha majengo ya  madarasa yalioenzuliwa na mvua  kali iliyonyesha  mwezi machi mwaka huu na kusabisha vifo vya watu sita na miundo mbinu mbalimbali  .
 Pia   aliishukuru  NMB  kwa  msaada wa  Kompyuta saba walizozitowa  ambapo wao  kama  Wilaya wamepanga   kuzipeleka  kwenye  Shule za  Sekondari za   Mamba ,Usevya na  Mbende.
Mkuu wa  Mkoa wa  Katavi  Raphael  Muhuga  alisema  Nmb  ndio    Benki  pekee  inayotowa  huduma za  kibenki katika   Wilaya ya  Mlele  na   aliiomba   benki hiyo  ifungue matawi  mengine  kwenye  Wilaya hiyo .
 Aliyataja  maeneo  ambayo  yanawatu  wengi na  mzunguko wa  fedha  ambayo  yanasitahili kuwa  na  huduma za  benki  hiyo kuwa ni  Maji moto  na usevya  katika  Wilaya ya Mlele na  Kasekese  Wiyani  Tanganyika .


No comments: