Mratibu
wa kampeni ya kuwezesha wanawake kutoka Oxfam Bi.Magdalena Thomas
akielezea kwa ufupi hali ilivyo katika suala zima la kuwawezesha
wanawake linavyohitaji nguvu zaidi huku akitolea mfano namna Mama Shujaa
wa Chakula ilivyofanikiwa kuleta mtazamo chanya na kufumbua macho
washiriki pamoja na jamii inayowazunguka.
Sambamba
na hilo aligusia safari iliyowahusisha washindi wawili wa Mama Shujaa
wa Chakula Bi. Elinuru Pallangyo mshindi wa mwaka 2014 pamoja na
Bi.Maria Mbuya mshindi wa mwaka 2016 ambao walizuru nchi za Uholanzi
pamoja na Italia na kukutana na wabunge nchini humo.
Mshindi
wa Mama Shujaa wa Chakula 2014 Bi. Elinuru Pallangyo akielezea namna
safari hii ilivyompa fursa ya kupaza sauti Kimataifa kueleza uhalisia
uliopo katika jamii ya Tanzania hasa katika sekta nzima ya kilimo na
namna wakulima wadogo hususan wanawake wanavyohitaji kushikwa mkono ili
kuboresha uzalishaji pamoja na kukuza kipato.
"Miongoni
mwa mambo niliyopazia sauti ni kuwahamasisha wenzetu walioendelea
kupitia mashirika pamoja na serikali kuja kuwekeza zaidi wakitulenga
wakulima wadogo wanawake kwani mchango wetu ni mkubwa lakini mazingira
siyo rafiki sana kuweza kutimiza malengo" alisema Bi.Elinuru.
Akizungumza
katika mkutano huo Mshindi wa Mama Shujaa wa Chakula mwaka 2016 alisema
yeye alijikita katika kuelezea changamoto zinazowakabili wanawake
katika uendeshaji wa kilimo nchini huku akianisha kuwa suala la umiliki
wa ardhi, wataalamu wa kilimo, miundombinu pamoja na mabadiliko ya tabia
nchi vimekuwa vikwazo vikubwa kwani wengi wakulima wadogo hasa wanawake
ni wenye mitaji midogo.
Naye Mratibu wa Kampeni ya chakula na mabadiliko ya tabia nchi kutoka Oxfam Bi. Nuria Mshare amesema Oxfam ni shirika la kimataifa linalofanya kazi katika nchi 90,ikiwemo Tanzania,ambapo lengo moja wapo ni kufanikisha mabadiliko endelevu kwa kuwainua wakulima wanawake wadogo kwa kuwasaidia katika sekta ya kilimo.
Sambamba
na hilo aliongeza kuwa miongoni mwa juhudi zinazofanywa na Oxfam ni
kushawishi serikali kuongeza bajeti katika wizara ya kilimo na pia
kuezidi kushawishi wawekezaji wa ndani na nje kuwekeza katika sekta ya
kilimo na hasa kwa wakulima wadogo.
Na Dickson Mulashani
No comments:
Post a Comment