Msanii maarufu nchini wa muziki wa bongo fleva Rehema Chalamila amesema watu wasimhukumu kwani alianguka kama binadamu wengine .
Ray C ameyasema hayo alipokuwa akifanya mahojiano katika kipindi cha Planet bongo kinachorushwa na kituo cha EATV .
''Nilianguka
bahati mbaya kama binadamu wengine ,nikajitambua sasa nipo vizuri
naendelea na maisha kama kawaida japo nakumbwa na changamoto ya kutopata
usaidizi kutoka kwa watu wangu wa karibu niliokuwa nao kwenye musiki
zamani''
Msanii
huyo amemshukuru Rais Mstaafu Jakaya Kikwete kwa kumchukulia kama
mwanae na kumsaidia kupata matibabu baada ya kutumia madawa ya kulevya
na kumuathiri kwa muda mrefu.
Aidha
ameiomba jamii kumpokea na kumuunga mkono katika kazi zake ambazo
anazifanya ambapo kwa sasa amerekodi nyimbo 5 na kuwataka waandaaji wa
vipindi vya redio,televisheni na magazeti badala ya kila siku kumuandika
vibaya wamuunge mkono katika jitihada zake za kurejea kwenye hali ya
kawaida.
''Kuna
magazeti kazi yao ni kuniandika vibaya kila siku mara nimeonekana
navuta madawa kwa nini wasinipige picha kama wananiona kuliko kuandika
uongo kila silku na kukatisha tamaa watu wenye lengo jema la
kunisaidia''.Amesema Ray C
No comments:
Post a Comment