Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo auHabari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @fredynjejeblog Twitter @Fredynjeje
Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), kwa kushirikiana na Taasisi binafasi
ya Karibu Tanzania Association (KTA) kwa pamoja wamezindua programu ya
maendeleo ya soka kwa wanawake vijana ili kuhamasisha usawa wa kijinsia,
uwezeshaji kijamii na kiuchumi kwa wanawake nchini itakayofadhiliwa na
Shirika la Forum Syd kutoka nchini Sweden.
Programu
hiyo inafadhiliwa na Shirika la Forum Syd la nchini Sweden imewekwa
saini na Katibu Mkuu wa TFF, Mwesigwa Selestine na Mia Mjengwa
Bergdahl, Mratibu wa Programu hiyo kutoka taasisi ya Karibu Tanzania
katika ofisi za TFF zilizopo Karume.
Awali
akizungumza Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania, Jamali Malinzi alisema
programu hiyo ni ya aina yake kwani haijawahi kufanyika nchini na
inalenga kujenga mfumo utakaotumiwa nchi nzima katika kutoa mafunzo kwa
soka la wanawake kwenye maeneo ya ufundi yaani makocha, waamuzi, uongozi
na tiba kwenye michezo.
“Programu
hii itasaidia kuendeleza vipaji kwa wachezaji wanawake na kuongeza hali
ya kujitambua na kujiamini kwa walengwa na lengo ni kuongeza idadi ya
wachezaji wenye ubora na viwango kwa soka la wanawake katika ngazi zote
hivyo programu hii ni nyenzo ya kuwawezesha wanawake,” alisema Malinzi.
Kozi
hii itakuwa inafundishwa katika vyuo 55 vya Maendeleo ya Jamii na kwa
kuanzia kozi 20 zitafundishwa katika vyuo 20 kwenye kanda saba.
Jumla ya wanawake 600 ikiwamo 30 kutoka katika kila vyuo vya Maendeleo ya Jamii watashiriki.
Katika
programu hii, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto wanashiriki kikamilifu kwa kuwezesha wanafunzi na miundo mbinu
ilivyo chini ya wizara hiyo kutumika katika kufanikisha programu hii.
Mafunzo
yatatolewa sambamba na mafunzo mengine ya kawaida yanayotolewa kwenye
Vyuo Vya Maendeleo ya Wananchi, kama vile maarifa ya jumla na mafunzo ya
ufundi.
No comments:
Post a Comment