Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo auHabari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @fredynjejeblog Twitter @Fredynjeje
Mahakama ya Haki za Binadamu ya Afrika
(AfCHPR) katika kikao chake kilichoanza jijini hapa, itapitia maombi ya
rufani ya mwanamuziki maarufu nchini, Nguza Viking na John Viking dhidi
ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Hata hivyo, taarifa iliyotolewa na
mahakama hiyo jana, ilieleza kuwa kesi hiyo namba 006/2015 iliyopangwa
kusikilizwa Machi 11 haitasikilizwa katika mahakama ya wazi.
Ni kesi mbili pekee kati ya 50
zitakazosikilizwa kwenye mahakama ya wazi, ikiwamo inayomhusu mwanasiasa
maarufu wa Rwanda, Victoire Ingabire aliyoifungua kupinga ukiukwaji wa
haki anaofanyiwa na Serikali yake.
Pia, mahakama ilieleza kuwa kikao hicho cha 40 cha kawaida kitakamilika Machi 18 na kutoa uamuzi wa mashauri manne
Kesi ya Ingabire inayotarajiwa kuvuta
hisia za watu wengi ikizingatiwa upinzani ambao amekuwa akiuonyesha
dhidi ya serikali yake, itasikilizwa Machi 4.
Katika kesi hiyo, Ingabire pamoja na
mambo mengine anadai haki zake kuvunjwa ambazo zinatajwa kwenye Mkataba
wa Mahakama hiyo Ibara ya 7, 10 na 18 hivyo anaitaka itoe uamuzi.
Pia, Taasisi ya Action Pour la
Protection des Droits de I’Homme (APDH) inaishtaki Serikali ya Ivory
Coast kuvunja mkataba wa Mahakama ya Afrika na Haki za Binadamu Ibara ya
3 na 17 katika kesi namba 001/2014, iliyopangwa kusikilizwa Machi.
Mahakama hiyo inaundwa na majaji 11
kutoka nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) na inakuwa na vikao vinne
kwa mwaka, kufikia Januari 31 tayari ilikuwa imepokea kesi 74 kati ya
hizo 25 imetolewa uamuzi.
Maombi manne yamepelekwa kwenye kwa uamuzi zaidi kwenye Kamisheni ya Afrika ya Haki za Binadamu.
Source:Mwananchi
No comments:
Post a Comment