Ikiwa unataka tengenezewa Blog, Tukiko lolote la Harusi,Msiba, Mahafali, Tamasha, Matangazo auHabari yoyote usisite kututumia kupitia whatsapp 0765056399 au Barua Pepe fredynjeje@live.com. Follow me instagram @fredynjejeblog Twitter @Fredynjeje
Kwa akili ya harakaharaka waliamua kuita bajaji ya mmoja wa
madereva wa pale kichochoroni ambao nao walikuwa wakiingiza kipato chao kupitia
machangudoa wa maeneo hayo kwa kuwasafirisha wateja wa biashara hiyo kutoka
sehemu moja hadi nyingine.
“Huu msala unajua!” alizungumza yule dereva kwa hamaki baada
ya kuambiwa kinachoendelea kuhusu yule mzee aliyezirai ghafla baada ya kupewa
penzi na Joy.
“Wewe kazi yako ni kumtupa tu huyu mzee mtaroni, kwani kuna
ugumu?” alisema Joy kwa woga.
“Nipe elfu ishirini,” aliongea yule dereva.
“Jamani punguzapunguza kidogo hapa ndiyo kwanza nilikuwa
naanza kazi, kaka angu,” alibembeleza Joy.
“Aah sista hiyo haipungui kabisa, hii kesi,” “Kaka angu,
naomba basi upokee hii, nisaidie kama mdogo wako,” alizidi kubembeleza Joy,
akatoa shilingi elfu 15 huku chozi likimtoka.
Yule dereva alimuonea huruma lakini alimpa sharti la kwenda
naye hadi sehemu yenye mtaro ili kumtupa yule mzee huyo maana yule dereva
alikuwa na wasiwasi kama msala utatokea.
Joy na dereva kwa kificho walimbeba yule mzee na kumuweka
kwenye siti ya nyuma ya bajaji, wakamkalisha upande wa kutokea, mwenyewe Joy
akiwa amemshikilia kiuno ili asidondoke.
Wakakata mitaa na kutafuta sehemu nzuri wamtupe, bahati
nzuri maeneo mengi yalikuwa hayana watu kutokana na muda kwenda sana.
Dereva na Joy wakamshusha yule mzee ambaye bado alionekana
kulegea vilivyo, wakamtelekeza pembezoni mwa barabara kisha wakageuza na
kuondoka.
Wakiwa umbali wa mita kadhaa Joy aligeuka na kutazama
kupitia kioo cha nyuma, akashtuka, akajikuta ameshika mikono kichwani
Huwezi amini yule mzee ambaye muda mchache uliopita
alionekana amezirai, alionekana amesimama na kukimbia tena huku akiwa anacheka
kwa sauti; “hahaa uroda burebure.”
Ni wazi kuwa Joy alikuwa ameingizwa mjini na yule mzee
ambaye alijifanya amezimia baada ya kufanya naye mapenzi, kumbe lengo lake
lilikuwa ni kutolipa hela yoyote baada ya huduma ya ngono.
Wakati yule dereva bajaji akiwa akicheka nusura mbavu
zivunjike kwa tukio lile, Joy alikuwa amekasirika kiasi cha kutosha, hasira
zilimpanda kwa hasara aliyokuwa ameingia; kwanza ametumika mwili wake bure
pasipo kupewa chochote, cha pili alikuwa amelipia elfu 15 nzima ya bajaji kwa
ajili ya kuutupa mwili wa mtu aliyedhani amezimia kumbe alikuwa ni tapeli.
Kwa huruma yake yule dereva bajaji aliamua kumrudishia
shilingi elfu 10 Joy na kuchukua elfu 5 akamrudisha pale kichochoroni kwa
machangu wenzake ambao mpaka muda huo wengine walikuwa wameshaenda na wateja
zaidi ya mara tatu na kuingiza mkwanja wa kutosha.
Kwa hasira Joy akaagiza kinywaji kikali cha Kiroba vipakiti
vitatu na kuvinywa harakaharaka. Vikamshusha hasira na kubust upya mudi yake.
Akasimama na kutega ndoano yake tena kwa mpita njia mmoja,
kijana mtanashati aliyeonekana akienda mbele lakini akili yake shingo yake
ikigeuka kama bundi akimtazama Joy kwa jinsi alivyoacha nusu na robo ya umbile
lake nje.
“Ni mteja mwenye aibu mfuate,” ni sauti iliyokuwa
ikizungumza ndani ya Joy, akaitii na kumfuata yule mtu, “kaka twende nikakupe
raha,” alisema Joy bila ya aibu;
“Shingi ngapi?” aliuliza yule kaka aliyeonekana mzoefu ila
mdhambi wa sirisiri maana aliongea akiwa gizani kweli.
“Elfu 10 kwa showtime, elfu 30 hadi asubuhi na unanishika
kokote unapopenda,” alijibu Joy macho yake yakiwa makavu kweli.
“Poa, twende,” alizungumza yule jamaa , Joy akamuongoza
kuelekea kwenye ile gesti yake ambayo muda mchache uliopita alikuwa amenusurika
kesi ya mauaji.
Nini kitafuatia Itaendelea kesho wala hautakiwi kukosa
No comments:
Post a Comment