Waziri
wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Harrison George Mwakyembe
akizungumza na waandishi wa habari Mjini Dodoma (hawapo Pichani) kuhusu
agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania la kuachiwa huru kwa
msanii wa Muziki wa kizazi kipya Emmanuel Elibariki (Ney wa Mitego)
Kulia ni Naibu Waziri wake Mhe. Anastazia Wambura.
Amshauri aboreshe wimbo wake zaidi.
Amesema ni haki yake ya kujieleza.
Na Raymond Mushumbusi WHUSM Dodoma
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli ameliagiza
Jeshi la Polisi kumwachia huru msanii wa muziki wa kizazi kipya Emmanuel
Elibariki maarufu kama Ney wa Mitego kutokana na wimbo wake Wapo
unaosadikiwa kukiuka madili.
Akitoa
kauli hiyo kwa niaba ya Rais Magufuli, Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa
na Michezo Mhe. Harrison George Mwakyembe amesema kuwa Msanii
huyo ametumia haki yake ya kikatiba ya kujieleza na ni Haki ya kila
Mtanzania kujieleza kwa namna moja au nyingine pasipo kuvunja katiba ya
Nchi.
Waziri
Mwakyembe amesema Mwanamuziki huyo ni Mmoja kati ya wanamuzi
wanaopendwa sana na Mhe Rais kutokana na kazi zake za muziki
zinazoelimisha na kueleza changamoto mbalimbali zinakumba taifa letu.
“Mhe.
Rais anaupenda wimbo wa msanii huyu na ameshauri auboreshe zaidi
asipunguze chochote ila aongezee tu tabia nyingine ambazo hajazitaja
katika wimbo wake” alisisitiza Dkt Mwakyembe.
Aidha
Mhe. Waziri ameeleza kuwa Mhe Rais ametoa ushauri kwa msanii huyo
kuboreshe wimbo huo zaidi kwani mengi aliyoyaongelea katika wimbo wake
yanatokea katika jamii na kutolea mfano kama akiboresha na kuelezea
zaidi kuhusu wakwepa kodi,wauzaji, wasambazaji na watumiaji madawa ya
kulevya,na watanzania wasipoenda kufanya kazi kwani makundi haya yote
yapo katika jamii.
No comments:
Post a Comment